TANGAZA NASISI

TANGAZA NASISI
bei zetu ni nafuu sanaaaaa

matangazo


Saturday, March 4, 2017

Je wajua

*TUJENGE MAGHOROFA !*
Kuna tofauti kubwa sana kati ya mtu anayejenga *GHOROFA* na yule anayejenga *Nyumba ya KAWAIDA.*
Anayejenga *Ghorofa* anatakiwa achimbe msingi Mrefu kwenda chini kabla hajaanza  
kuinua *Ghorofa* yake juu. Hivyo wakati huyu mwingine anapokuwa anajenga Nyumba ya kawaida atakapokuwa tayari anakaribia hata kuezeka, unaweza kukuta yule anayejenga *Ghorofa* bado yuko kwenye Msingi.
Ila siku akianza kuinua *Ghorofa* lake,  kila mtu atashangaa urefu wa juu atakaoenda nao.
Kwenye maisha ndivyo ilivyo- *"If want to go so high, you need to go so deep"*_*(Kama unataka kwenda juu sana ni lazima ukubali kwenda chini sana).*_ Ni lazima ufanye kitu cha  tofauti kitakochokujengea _*Future imara.*_
Ukweli ni kuwa Watu wengi wanaokuzunguka wanajenga maisha ambayo ni kama *Nyumba ya kawaida.*
Na wewe kama unataka kujenga maisha yanayofanana na *Ghorofa,*
Ni lazima ukubali kuonekana unachelewa kwenye baadhi ya mambo.
Hii inamaanisha nini?...
Hii inamaanisha kuwa utalazimika kufanya vitu vya *TOFAUTI* na kuwa *TAYARI* kusubiri.
Utatakiwa *Kuwekeza* wakati wengine wanaenda kununua nguo mpya  waendane na Fashion,
Utatakiwa *Kusoma vitabu* wakati wengine wanaangalia movie na kupiga stories,
Utatakiwa *Uanzishe Biashara yako* wakati wenzako wamesharidhika na mshahara  wanaopata n.k
Unachofanya kuanzia unapoamka hadi unapoenda kulala kitajulisha kama unajenga *Maisha GHOROFA* ama *Maisha KAWAIDA.*
Ukijiona unapoteza muda hovyo,
ukiingia *Facebook/instagram* ni kusoma umbea tu,
Unalalamika unasema utafanya na hakuna unachofanya, ujue unajenga *Maisha ya KAWAIDA* tena ni kama *Nyumba ya UDONGO.*
Ukitaka kujenga maisha *GHOROFA;*
*1.* _Jifunze kitu kipya leo._
*2.* _Chukua hatua kuelekea Ndoto yako._
*3.* _Usiwe mtu wa kulalamika bali tafuta suluhisho kwa kila changamoto._
Je, LEO utajiunga na wanaojenga *Maisha GHOROFA* ama wale wanaojenga *Maisha ya KAWAIDA?*
Twende zetu tujenge *Maghorofa !!!*

No comments:

Post a Comment